|
|
“Dear children, To come to you and to make myself known to you is a great joy for my motherly heart. It is a gift from my Son for you and for others who are coming. As a mother I am calling you: love my Son above everything. In order to love Him with all your heart, you need to come to know Him. You will come to know Him through prayer. Pray with the heart and with your feelings. To pray means to think of His love and sacrifice. To pray means to love, to give, to suffer and to offer. I am calling you, my children, to be apostles of prayer and love. My children, it is a time of vigilance. In this vigil I am calling you to prayer, love and trust. As my Son will be looking in your hearts, my motherly heart desires for Him to see unconditional trust and love in them. The united love of my apostles will live, will conquer and will expose evil. My children, I was a chalice of the God-man; I was God's instrument. That is why I am calling you, my apostles, to be a chalice of the true and pure love of my Son. I am calling you to be an instrument through which all those who have not come to know the love of God-who have never loved-may comprehend, accept and be saved. Thank you, my children. ”
|
|
|
“Wanangu wapendwa, nikiwatazama hapa mmekusanyika kunizunguka, Mama yenu, ninaona nafsi safi nyingi. Ninawaona wanangu wengi wanaotafuta upendo na faraja lakini hakuna mtu anayewapa. Ninawaona hata wale wanaotenda mabaya maana hawana mifano myema, maana hawajamjua mwanangu. Mwanangu anawatuma ninyi kwangu, Mama, sawa kwa wote, niwafundisheni kupenda, ili muelewe ya kuwa ninyi ni ndugu. Ninatamani kuwasaidia. Mitume wa upendo wangu, kwa mwanangu yamtosha tamaa hai ya imani na upendo na atayakubali, lakini mnapaswa kustahili, kuwa na tamaa na mioyo wazi, Mwanangu huingia katika mioyo wazi. Mimi kama Mama ninatamani kwamba mjue Mwanangu katika kweli: Mungu aliyezaliwa na Mungu, kwamba mjue ukuu wa Upendo wake, ambao mnahitaji. Yeye amezichukua juu yake dhambi zenu, ameupata Ukombozi wenu, na badala yake anaomba mpendane ninyi kwa ninyi. Mwanangu ni upendo, Yeye anawapenda watu wote bila tofauti, watu wote wa nchi zote, wa mataifa yote. Ikiwa ninyi, wanangu, mngeishi upendo wa Mwanangu, ufalme wake ungekwisha kuwa duniani. Kwa hiyo, Mitume wa upendo wangu, salini, salini ili Mwanangu na upendo wake wawe ndani yenu nanyi muweze kuwa mfano wa upendo na muweze kuwasaidia wote wale ambao hawajamjua Mwanangu. Msisahau kamwe kwamba Mwanangu, mmoja na utatu, anawapendeni. Pendeni na wombeeni wachungaji wenu. Nawashukuru. ”
|