|
|
Ikiwa unaona ujumbe kutoka kwa mtu unayemfahamu ambao hauonekani kama aina ya ujumbe anaoweza kutuma, huenda akaunti yake imevamiwa na mhalifu wa mtandaoni ambaye anajaribu kupata pesa au maelezo kutoka kwako - hivyo kuwa mwangalifu jinsi unavyojibu. Mbinu za kawaida ni pamoja na kukuuliza umtumie pesa kwa dharura, akidai ametelekezwa katika nchi nyingine au akisema kuwa simu yake imepotea ili asipigiwe. Ujumbe huo pia unaweza ukakwambia ubofye kwenye kiungo ili uone picha, makala au video, ambacho kwa kweli kitakuelekeza katika tovuti ambayo inaweza kukuibia maelezo yako - kwa hivyo usibofye tu, fikiria kwanza!
|