|
|
Pindi tu unapounda nenosiri la Akaunti yako ya Google, tunakuhimiza uongeze safu ya ziada ya usalama kwa kuwezesha uthibitishaji wa hatua mbili. Uthibitishaji wa hatua mbili unakuhitaji kufikia simu yako, pamoja na jina lako la mtumiaji na nenosiri, unapoingia. Hii inamaanisha kuwa ikiwa mtu fulani ataiba au kudadisi nenosiri lako, mwingiaji kwenye akaunti bila idhini aliyepo bado hawezi kuingia kwenye akaunti yako kwa sababu hana simu yako. Sasa unaweza kujilinda kwa jambo ambalo unajua ( nenosiri lako) na jambo ulilo nalo (simu yako).
|