|
“Wanangu, ninawaomba kuwa hodari wala kutowayawaya, maana hata mema madogo zaidi, ishara ya upendo mdogo zaidi hushinda maovu yanayoonekana zaidi na zaidi. Wanangu nisikilizeni ili mema yashinde, ili muweze kujua upendo wa Mwanangu ulio furaha mkubwa zaidi kuliko zote. Mikono ya mwanangu inawakumbatia, Yeye, apendaye nafsi, Yeye ambaye amejitolea kwa ajili yenu na kunajitolea sikuzote tena katika Ekaristi, Yeye aliye na maneno ya Uzima wa milele; kujua upendo wake, kufuata hatua zake, maana yake ni kuwa na mali ya kiroho. Huo ni utajiri unaojaza hisia iliyo njema, na unaoona upendo na mema popote. Mitume wa upendo wangu, wanangu, muwe kama mionzi ya jua ambayo kwa joto la upendo wa Mwanangu inawapasha joto wote wale wanaoizunguka. Wanangu, ulimwengu unahitaji mitume wa upendo, ulimwengu unahitaji sala nyingi, lakini sala zinazosaliwa kwa moyo na roho, si kwa midomo tu. Wanangu, muwe na hamu ya utakatifu mkiwa na unyenyekevu unaomwezesha Mwanangu kufanya kazi kwa njia yenu, kama Yeye apendavyo. Wanangu, sala zenu, fikira zenu na matendo yenu, haya yote yawafungulia ama kuwafungia mlango wa Ufalme wa Mbinguni. Mwanangu aliwaonyesha njia na kuwapa tumaini, mimi ninawafariji na kuwapa moyo maana, wanangu, mimi nilijua maumivu, lakini nilikuwa na imani na tumaini, sasa nimepata thawabu ya uzima katika Ufalme wa Mwanangu. Kwa hiyo, nisikilizeni, jipeni moyo, msiwayawaye. Nawashukuru. ”
|
|
«Chers enfants, je vous invite à être courageux, à ne pas défaillir, car même le bien le plus petit, le signe d'amour le plus léger, est vainqueur du mal qui est de plus en plus visible. Mes enfants, écoutez-moi afin que le bien prédomine, afin que vous puissiez connaître l'amour de mon Fils. Voilà le plus grand bonheur : les bras de mon Fils qui vous étreignent, lui qui aime l'âme, lui qui s'est donné pour vous et qui se livre toujours à nouveau dans l'Eucharistie, lui qui a les paroles de la vie éternelle. Connaître son amour, suivre ses traces, signifie avoir une vie spirituelle riche. Cette richesse donne de bons sentiments et voit partout l'amour et la bonté. Apôtres de mon amour, mes enfants, vous êtes comme les rayons du soleil qui, par la chaleur de l'amour de mon Fils, réchauffent tous ceux qui les entourent. Mes enfants, le monde a besoin d'apôtres de l'amour, il a besoin de beaucoup de prière, mais d'une prière dite avec le cœur et avec l'âme, et pas seulement prononcée avec les lèvres. Mes enfants, recherchez la sainteté, mais dans l'humilité. L'humilité qui permet à mon Fils de faire, à travers vous, ce qu'il désire. Mes enfants, vos prières, vos paroles, vos pensées et vos actes, voilà tout ce qui vous ouvre ou vous ferme les portes du Royaume des Cieux. Mon Fils vous a montré le chemin et vous a donné l'espérance, et moi, je vous console et vous encourage. Car, mes enfants, j'ai connu la souffrance, mais j'avais la foi et l'espérance. Maintenant, j'ai la récompense de la vie dans le Royaume de mon Fils. C'est pourquoi, écoutez- moi, prenez courage, ne défaillez pas ! Je vous remercie! »
|